Wataalamu
mbalimbali wamefasili maana ya fasihi simulizi katika mitazamo tofauti tofauti
kama ifuatavyo-;
Balisdya(1983)
Fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa
,kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake.
Msokile,M(1992).
Fasihi simulizi ni kazi ya sanaa inayotumia lugha .Kazi hii huhifadhiwa kwa
kichwa na kusambazwa kwa njia ya masimulizi ya mdomo ,hurithishwa kizazi hadi
kizazi.
Fasihi
simulizi ni sanaa inayotumia lugha ya mazungumzo
ya ana kwa ana ,sauti na vitendo na njia zote za mawasiliano kufikisha ujumbe kwa jamii.
Massamba(2003)akimunukuu
Shaaban Robert anasema ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama
nyimbo,mashairi na tenzi zaidi ya kuwa sanaa ya vina unaufasaha wa maneno
machache au muhtasari.
Mnyampara
(1970) anasema kuwa ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale ndicho
kitu kilicho bora sana ,maongozo ya dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha
nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa vina na mizani maalumu.
Ushairi
ni kazi ya sanaa yenye kuandikwa au kuimbwa kwa kufuata kanuni za ushairi au
kutofuata kanuni za ushairi ikiwa na maana kuwa ushairi waweza kuwa wa
kimapokeo au wa kisasa ilimradi ushairi huo uwe unaimbika.
Ushairi
kama tanzu mojawapo ya fasihi simulizi haukutoka kwenye ombwe tupu bali una
chimbuko lake ambalo huweza kutueleza
jinsi ulivyoanza,kukua na kuenea katika sehemu mbalimbali
Chanzo
cha mashairi ni mabadiliko ya kihistoria ya jamii, kisiasa,kiuchumi na
kiutamaduni mfano nchini Tanzania matukio kama vile kipindi cha uhuru,azimio la
Arusha ,vita vya Kagera ,mfumo wa vyama vingi yamezaa ushairi wa fasihi
simulizi ambao unayaelezea matukio hayo kwa undani na athari zake kwa jamii.
Migongano ya kitabaka katika jamii nayo ni chanzo mojawapo cha ushairi katika
kutatua migogoro hiyo ,watu huzua ushairi unaolingana na hisia zilizo katika
mazingira yao. Vilevile shughuri mbalimbali za kijamii kama vile dini ,harusi,
sherehe mbalimbali ,misiba zinazua ushairi wake unaolingana na shughuli hizo za
kijamii hali ambayo imepelekea kuwa na nyimbo za kanisani ,harusini, jando na
unyago na maombolezo.
Sayansi
ni mfumo wa kutolea maarifa katika jamii
kupitia kuona na kutenda ilihali teknolojia ni uwasilishwaji wa sayansi hiyo.
Hakuna
jambo nzuri lililotokea duniani bila ya kuwa na athari zake .Mafanikio haya ya
sayansi na teknolojia mpya yameleta athari kubwa sana katika fasihi simulizi na
tanzu zake zote hususani utanzu wa ushairi na vipera vyake kama ifuatavyo;-
Nyimbo
ni sanaa yenye dhima kubwa katika jamii ,hutumika kuburudisha watukwenye sherehe
au wakati wa mapumziko ,kuonya ,kufunza, kuarifu kunogesha hadithi,kuomboleza
,kubembeleza mtoto ili alale,kuchapua kazi na kutia hamasa vitani .Nyimbo hizi
zilianza kutumika toka binadamu alipoanza kupambana na mazingira yake. Shughuli mbalimbali za uzalishaji mali pamoja na
shughuli za kijamii ziliwafanya watu waibue nyimbo mbalimbali kutokana na hisia
za kibinadamu katika kutaka kutawala jamii yake na shughuli zake za kila
siku.Kabla ya kuja kwa wakoloni na maendeleo ya sayansi na teknolojia tulikuwa
na nyimbo zetu za asili ambazo ziliimbwa kufuatana na kazi waitendayo kwa lengo
la kuchapuza kazi hiyo .Kila kazi katika enzi za mababu zetu ilikuwa na nyimbo
zake , mfano kilimo(wawe),kutwanga,kupepeta,kusuka,kuchuuza,useremala,uvuvi,ubaharia(kimai),uashi,ufugaji,ufuaji
chuma na uhunzi.Pia kulikuwa na nyimbo
za watoto kwa lengo la kubembeleza watoto wakati mama afanyapo kazi ambapo nyimbo hizo zilikuwa na uwili ambapo maudhui
yalikua ya kiutu uzima na fani ilikuwa ya kitoto.Kila kabila ilikuwa na aina
yao ya kubembeleza watoto vile vile
kulikuwa na nyimbo ambazo ziliimbwa wakati wa kupeleka vijana jandoni na
unyagoni.Lengo la nyimbo hizi ni kuwatia moyo na kuwapa ushupavu na ujasiri.Pia
kusisitiza dhima mpya ya kiutu uzima na kuuaga utoto,mfano wa wimbo wa jando uliokuwa ukiimbwa zamani
‘’Netumwa kiazi
tungu
Nachimba cha
mnyelele
Kizongozongo mabuyu
Ndani kinauchelele
Ukikichocha hakigwi
Kitunga
mambelembele
Kitamu
sili na ndugu
Jirani
simtoche(le)
Kitiwacho sitarani
Funga
na lengo komele……’’
Kutokana
na kuibuka kwa sayansi na teknolojia
nyimbo zimepoteza uasiliawake kutokana na kuwepo kwa vifaa vya kisasa.Nyimbo
zimeathiriwa na sayansi na teknolojia mfano badala ya mama kumbeba mtoto mgongoni na
kumbembeleza ili alale, kumeibuka
vifaa mbalimbali vya kubembeleza
watoto. Vifaa hivi vinafanya kazi aliokua akiifanya mama kwa mtoto, mfano wa
vifaa hivyo ni baisikeli ,simu, filimbi
,vinanda, bembea na mwanasesele. Vifaa hivi
vimeathiri na kupoteza uasili wa nyimbo zetu ambazo zilikuwa zikitumiwa
na mama zetu katika kubembeleza watoto.Pia uwepo wa sayansi na teknolojia umesababisha
kuongezeka kwa maradhi ambayo yamepelekea shughuri za jando na unyago
kufanyikia Hospitalini na kupelekea kutoweka kwa nyimbo ambazo zilikuwa zikiimbwa katika shughuli hizo za jando na unyago. Uwepo wa
sayansi na teknolojia umeleta athari pia katika nyimbo za maombolezo ambapo
badala ya watu kukaa na kumfariji mfiwa kwa kutumia nyimbo za asili sasa watu
hutumia luninga ,nyimbo za dini
mbalimbali au hata nyimbo za bongo fleva.
Ushairi
ni utanzu wa fasihi simulizi unaowasilishwa kwa hadhira kwa njia ya uimbaji au
ughani badala ya usemaji wa kawaida. Vigezo vilivyotumika katika kugawa utanzu
huu ni kigezo cha lugha ambacho ni lugha ya kishairi. Kigezo cha pili ni fani ambayo fani
iliyotumika ni wizani,lugha ya mkato, lugha ya mafumbo na uimbaji au ughani .Katika
utanzu huu kuna vipera viwili ambavyo ni nyimbo na maghani .Kabla ya ukuaji wa
sayansi na teknolojia mashairi yalitambulika kupitia sifa zake bainifu ambazo
ni urari wa vina na mizani na urari wa mapigo, hivyo ilimlazimu mtunzi wa
mashairi kutumia sifa hizo katika kutengeneza kazi yake ya fasihi na mashairi
yaliyokuwa yakitungwa yalikuwa yakisifia utawala, mambo ya kishujaa
yaliyofanyika katika jamii, kutoa wosia kwa vijana ,kuhamasisha jamii na
mshairi alisifika kutokana na ufundi wake wa kutunga na kughani mashairi. Mfano
Lakini
kwa sasa kutokana na ukuaji wa sayansi na teknolojia, sifa za urari wa vina na mizani si muhimu kilicho muhimu ni
maudhui yanayozungumuziwa ndani ya ushairi au maghani .Hii ni kutokana na
kuongezeka kwa washairi ambao wamekuja na mfumo mpya wa utungaji wa mashairi
bila kuzingatia urari wa vina na mizani .Mfano waimbaji wa muziki wa kizazi kipya ambao hutunga mashairi mengi
yanayojali maudhui bila kuzingatia urari
wa vina na mizani .Ukweli huu unadhibitika katika shairi la ‘’Ndiyo mzee’’ liliyoandikwa na Professor Jay
‘’OK,
OK naitwa Joseph Haule mwana Msolopaganzi
Nadhani
nimeletwa kuokoa hiki kizazi
Mimi
ni mwanasiasa aliyebarikiwa na Mungu
Nimeletwa
kwenu waungwana niwapunguzie machungu
Mimi
ni mteulekusini mwa jangwa la sahara
Ndio
maana nimetunukiwa cheti cha juu cha
utawala
Nina
hekima kuliko mfalme suleimani msiwe na wasi
Na
hii nitadhihirisha pindi mtakapo nipa nafasi
Actually
nimedhamiria kuwasaidia
Taifa
lenye nguvu duniani liwe ni Tanzania.’’
Katika kipindi cha awali uhifadhi wa mashairi kama
kazi ya sanaa ulikuwa katika ubongo wa fanani ,ambapo fanani katika utendaji wa
kazi yake alionana ana kwa ana na
hadhira na uwepo wa hadhira ulipelekea utendaji wa kipera hiki kuwa hai.
Lakini katika kipindi hiki cha maendeleo ya sayansi na teknolojia kazi
hii ya kisanaa haihifadhiwi katika kichwa cha fanani bali huhifadhiwa katika
vyombo vya kisasa kama vile vinasa sauti,tanakilishi ,CD za picha na maandishi
hivyo si lazima fanani kuonana na hadhira.
Maghani
ni ushairi unaoganwa au kuimbwa hadharani. Mara nyingine sauti ya maghani huwa ni
kati ya uzungumzaji na uimbaji .Katika enzi za mababu zetu maghani zilikuwa za
masimulizi na zilitambwa hadharani pamoja na ala ya muziki kama, vile ngoma na
marimba na zilitambwa bila ala ya muziki. Maghani hizi zilizungumzia masuala mazito
ya kijamii au ya kibinafsi na zilikuwa ndefu sana zenye kusimulia hadithi au
historia, zilikuwa zimegawanyika katika ghani za nafsi ,ghani tumbuizo ,sifo na
ghani masimulizi. Maghani Hizi zote
zilikuwa zikielezea masuala mbalimbali yaliyokuwa yakitokea katika jamii .Mfano
wa maghani sifo walizokuwa wakitumia mababu zetu ni zile za Fumo lyongo na
Mwanakupona. Mfano wa maghani ya Fumo
lyongo ni kama vile;-
‘’Lyongo
kitaka mali
Akababalighi
rijali
Akawa
mtu wa kweli
Na
haiba kuongeya
Wagala
wakabaini
Kumwambia
sulutwani
Twamtaka
kwa thamani
Kijana
kutuweleya
Twaitaka
mbeu yake
Nasi
kwetu tuipeke
Kwa
furaha tumuweke
Apate
kutuzaliya’’
Kutokana
na maendeleo ya sayansi na teknolojia mfumo wa utambaji wa maghani wa zamani
umepoteza uhalisia wake, kwa sasa mghani hurekodi mapigo mbalimbali
yanayoendana na kazi yake. wakati wa kughani mghani huhitaji mapigo au ala yaliyorekodiwa na kuhifadhiwa
kwenye vyombo vya kisasa kama vile santuri na kanda za kunasia sauti ambazo
humurahisishia mghanaji (mghani) kufanya kazi yake vizuri. Mfano wimbo wa
‘’Nikipata nauli’’ uliotungwa na Mrisho Mpoto.
Pole
sana mjomba
Kwa
kibarua kizito
’cha
kutaka kubadili
Dunia
kuwa kijiji
Hongera
Kile
kiitikio cha
Globalization
kimeimbwa
Vizuri
sana,japo
Hakijakaririwa
Na
sikia wageni wamefurahi
Sana
na ule ubeti wa mwisho
Uliouongeza
wa mbio zetu
Toka
uhuru mpaka hapa tulipo’’
Ngonjera
ni tungo za kishairi ambazo huwa na muundo wa majibizano. Utungo huwa ni
wakimazungumzo unaoweza kuhusisha malumbano au kujibizana kwa nia ya kutoa
ujumbe Fulani. Mhusika mmoja anaweza kusana jambo moja katika ubeti mmoja na
mwingine kujibu. katika jamii za kiafrika kuna aina ya ushairi wa fasihi
simulizi unaoweza kuhusihwa na ngonjera
ambapo mtunzi mmoja husema jambo ambalo wenzake wanaliendeleza. Kwa njia
hii kunakuwa na aina ya majibizano kati ya wahusika, mfano ngonjera zilikuwa
zikiimbwa katika sehemu za pwani hasa
Lamu na Zanzibar pia jamii nyingine ziliimba ngonjera sehemu mbalimbali kama
vile harusini, katika sherehe za kiutamaduni na ngonjera hizo ziliwasilishwa
kwa njia ya mdomo. Katika kipindi cha mababu zetu ngonjera hizi ziliimbwa
katika mazingira halisi yaliyohusisha fanani na hadhira walikuwa wakionana ana
kwa ana wakati wa uimbaji wa ngonjera. Kutokana na uwepo wa sayansi na
teknolojia ngonjera hizi za zamani
zimepoteza hadhi yake na kupoteza uhalisia wa kiafrika hali ambayo zimebadilika
na kuchukua uhalisia wa kizungu. Pia
ngonjera za siku hizi zinaimbwa kwa ajili ya kuendeleza siasa na mapenzi.
Kwa
ujumla ushairi huweza kufa kutokana na mabadiliko ya kijamii, kisiasa kiuchumi
na kiutamaduni. Mabadiliko hayo husababisha kitu cha zamani kife au kitu kipya
kiibuke kutokana na hali hii sayansi na teknolojia imesababisha nyimbo za
zamani kufa kutokana na muda wake kupita au kuisha na badala yake zimeibuka
nyimbo mpya katika tasinia ya leo.